Sura ya Kwanza
Ukoloni katika Jamii za Kitanzania
Utangulizi
Kipindi ukoloni unaingia, jamii nyingi za Kitanzania zilikuwa zimepiga hatua katika maendeleo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Katika sura hii, utajifunza kuhusu chimbuko, ukuaji, mifumo na mchango wa ukoloni katika uhusiano wa Tanzania na mataifa yaliyoitawala. Umahiri utakaoufunga utakuwezesha kuthamini maendeleo ya jamii za Kitanzania katika kipindi cha ukoloni. Pia, utaweza kushiriki vyema katika juhudi za kuleta maendeleo ya Tanzania.
Fikiri
Hali ya jamii za Kitanzania wakati ukoloni unaingia.
Chimbuko na Ukuaji wa Ukoloni
Ukoloni ni hali ya nchi moja kuitawala nchi nyingine katika nyanja zote za kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni. Katika muktadha huu, uchumi, siasa na utamaduni wa nchi zinazotawaliwa hutumiwa kwa malengo ya wakoloni. Ukoloni ulitokana na kustawi kwa mfumo wa ubepari, ambao ulifikia hatua ya ubeberu huko Ulaya Magharibi.
Ukuaji wa ubepari katika robo ya mwisho ya karne ya 19 uliambatana na mapinduzi na maendeleo ya viwanda katika nchi za Ulaya Magharibi. Maendeleo hayo ya viwanda yalisababisha ongezeko kubwa la mahitaji ya malighafi hasa za kilimo na madini kwa ajili ya uzalishaji viwandani.
Baada ya nchi za Ulaya Magharibi kutuma wapelelezi miaka ya 1850 hadi 1870 waligundua kuwa Bara la Afrika lina uwezo wa kuzalisha malighafi za kutosha kwa ajili ya viwanda vya Ulaya Magharibi. Mataifa kama Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Ubelgiji na Ureno yalivutiwa na rasilimali hasa ardhi yenye rutuba, misitu, mito, wanyama pori na madini barani Afrika.
Sababu za Uvamizi wa Kikoloni
Wakati huo huo, mataifa haya yalihitaji masoko mapya kwa bidhaa zilizozalishwa na viwanda vyao na hivyo makoloni yalionekana kama masoko mapya ya bidhaa za viwandani. Pia, mataifa haya yalihitaji maeneo ya kuwekeza mitaji yao ili kupata faida kubwa.
Kulikuwa pia na ushindani wa kisiasa na kijeshi kati ya mataifa ya Ulaya Magharibi kutawala maeneo makubwa. Lengo liikuwa ni kudhihirisha nguvu zao za kiuchumi na kijeshi na hasa kutawala sehemu muhimu za kimkakati.
Vilevile, kulikuwa na matamanio makubwa ya kueneza dini ya Kikristo, kwani wamisionari waliona ni wajibu wao kueneza maadili ya Kikristo katika maeneo mbalimbali, hasa barani Afrika.
Mbinu za Kuanzisha Ukoloni
Wakoloni walitumia mbinu mbalimbali kuanzisha na kuimarisha tawala zao. Mbinu hizo ni pamoja na mikataba ya kilaghai, kutumia viongozi wa jadi ili angalau kupata ushawishi na hatimaye kuzitawala jamii hizo.
Moja ya mikataba ya kilaghai iliyosainiwa ni ule wa kati ya Chifu Mangungo wa Usagara na Karl Peters, mwakilishi wa Wajerumani mwaka 1885. Mkataba huo uliruhusu matumizi ya ardhi ya Usagara na uliweka msingi wa kukua na kuenea kwa ukoloni wa Kijerumani katika maeneo yaliyoitwa Afrika Mashariki ya Kijerumani.
Wakati mwingine ukoloni ulikuwa na kuenea kwa kutumia nguvu za kijeshi. Maeneo ambayo wenyeji walipinga uvamizi walishindwa kutokana na sababu mbalimbali, ikiwemo ubora wa silaha za wakoloni ukilinganisha na silaha za jadi zilizotumiwa na jamii za Kitanzania.
Zoezi la 1.1
- Kwa nini Waingereza walibadilisha mfumo wa utawala kutoka utawala wa moja kwa moja hadi mfumo wa uwakala?
- Eleza jinsi mifumo ya utawala wa Waarabu, Wajerumani na Waingereza ilivyoyaathiri maendeleo ya jamii za Kitanzania.
- Tofautisha mifumo ya utawala wa Waarabu, Wajerumani na Waingereza katika Tanzania.
Mifumo ya Kikoloni ya Mataifa Yaliyozitawala Jamii za Kitanzania
Utawala wa Waarabu
Waarabu kutoka Oman walifika Zanzibar na Tanganyika mwishoni mwa karne ya 18. Kwa madhumuni ya kutawala, walijenga makazi yao katika maeneo ya Unguja, Pemba na pwani ya Tanganyika, hususani katika miji ya Kilwa, Tanga na Bagamoyo.
Kielelezo 1.2: Maeneo ambayo Waarabu waliweka ngome za utawala wao
Maeneo ambayo Waarabu waliweka ngome za utawala wao
Watawala wa Kiarabu waliotawala pwani ya Afrika Mashariki walifika nehini katika vipindi mbalimbali. Wengi wao walivutiwa na utajiri wa rasilimali uliokuwapo katika eneo hili. Utajiri huo ulijulikana kutokana na uhusiano wa kibiashara wa muda mrefu kati ya pwani ya Afrika Mashariki na nchi za bara la Asia kama vile Omani, Uhindi, Uchina na Uajemi.
Mtawala wa kwanza wa Kiarabu katika eneo hili alijulikana kama Sultani Seyyid Said bin Sultan. Sultani huyu alikuwa Mwarabu wa kwanza kutawala kwa pamoja dola za Omani na Zanzibar, kuanzia mwanzoni mwa miaka ya 1800 hadi alipofariki dunia mwaka 1856.
Utawala wa Wajerumani
Wajerumani walitawala jamii za Kitanzania kuanzia mwaka 1885 hadi 1919 baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Katika utawala wao, Wajerumani walitumia mfumo wa utawala wa moja kwa moja, uliokuwa na matumizi ya nguvu za kijeshi na sheria kali dhidi ya watawaliwa.
Jamii nyingi za Kitanzania ziliporwa ardhi na kulazimishwa kufanya kazi katika mashamba na miradi ya kikoloni kama vile ujenzi wa reli na miundombinu mingine kwa ujira mdogo. Wajerumani walitawala nyanja zote za maisha ya Waafrika huku wakiendeleza miundombinu kwa ajili ya masilahi yao.
Utawala wa Waingereza
Waingereza walitawala Tanganyika kuanzia mwaka 1919 hadi 1961. Baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, Tanganyika iliwekwa chini ya udhamini wa Jumuiya ya Mataifa (League of Nations) na baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia, chini ya Umoja wa Mataifa (United Nations Organisation).
Kuanzia mwaka 1919 hadi 1925, Waingereza waliendeleza muundo wa utawala waliourithi kutoka kwa Wajerumani. Hata hivyo, kuanzia mwaka 1926, chini ya uongozi wa Gavana Sir Donald Cameron, Waingereza walibadilisha mfumo huo na kuanzisha utawala wa kiuwakala.
Kielelezo 1.1: Gavana Sir Horace Byatt
Gavana Sir Horace Byatt
Kazi ya Kufanya 1.1
Umeteuliwa kuwa miongoni mwa wanafunzi watakaoshiriki mdahalo wenye mada isemayo "Ukoloni ulikuwa na manufaa katika maadili ya jamii za Kitanzania." Soma vitabu na matini mbalimbali kisha andaa dondoo utakazozitumia wakati wa mdahalo huo.
Mchango wa Ukoloni katika Uhusiano wa Tanzania na Mataifa Yaliyoitawala
Kabla ya ujio wa wakoloni, jamii za Kitanzania zilikuwa na uhusiano wa kuheshimiana na kushirikitana na jamii nyingine za Afrika na kwingineko. Uhusiano huu ulijengwa kwa misingi ya biashara, ambapo jamii hizo zilibadilishana bidhaa kama vile dhahabu, pembe za ndovu na vyakula.
Hali hii ya ushirikitano ilianza kubadilika baada ya ujio wa wakoloni kutoka Ulaya Magharibi. Mataifa ya Ulaya, hususani Ujerumani na Uingereza, yalitawala maeneo mbalimbali kwa lengo la kunyonya rasilimali za jamii za Kitanzania.
Baada ya ukoloni kushamiri, uhusiano kati ya jamii za Kitanzania na wakoloni uliingia katika hali ya uhasama mkubwa. Mataifa ya kikoloni ya Ulaya Magharibi yalitumia mbinu za kijeshi na kisiasa kutawala jamii za Kitanzania.
Ukoloni uliathiri kwa kiasi kikubwa uhusiano wa kijamii na kiuchumi wa jamii za Kitanzania. Uhusiano wa kibiashara uliokuwa na mafanikio zamani sasa ulibadilika na kuwa wa kiunyonyaji.
Mbali na uhasama, ukoloni pia ulileta athari kubwa kwenye utamaduni na mifumo ya kijamii. Utamaduni wa kigeni ulienea katika jamii za Kitanzania na kudhoofisha utamaduni na maadili ya asili.
Ingawa ukoloni ulisababisha uhusiano mbaya baina yake na jamii za Kitanzania, pia ulisababisha mwamko mpya wa utaifa wa kudai uhuru. Harakati za kudai uhuru na kujikomboa zilichochea umoja miongoni mwa jamii za Kitanzania.
Zoezi la Marudio
- Eleza sababu za wakoloni kutoanzisha viwanda vya kuzalisha bidhaa katika maeneo ya Tanzania wakati wa ukoloni.
- Linganisha hali ya utoaji wa huduma za jamii wakati wa utawala wa Wajerumani na Waingereza katika jamii za Kitanzania.
- Fafanua namna ambavyo sera za utawala wa Wajerumani na Waingereza zilivyokinzana na maadili ya jamii za Kitanzania.
- Jamii za sasa za Tanzania zinaweza kujifunza nini kuhusu usimamizi wa rasilimali na utawala kutoka kwa Wajerumani na Waingereza?
- Kwa kurejelea utoaji wa huduma za kijamii wakati wa ukoloni, pendekeza namna bora ya kuboresha utoaji wa huduma za kijamii katika Tanzania ya sasa.
- Tofautisha utoaji wa huduma za jamii wakati wa sasa na ule wa utawala wa Wajerumani na Waingereza.
Sura ya Pili
Athari za Ukoloni katika Maadili ya Kitanzania
Utangulizi
Kuingia kwa ukoloni mwishoni mwa karne ya 19 kulisababisha kuanza kupepea kwa maadili ya kikoloni, ambayo yalilidhoofisha mifumo asilia ya maadili ya jamii za Kitanzania. Katika sura hii, utajifunza kuhusu dhana ya maadili katika kipindi cha ukoloni na maadili ya jamii za Kitanzania wakati wa kuingia kwa ukoloni. Mlevile, utajifunza athari za mfumo wa ukoloni katika maadili ya Kitanzania na maadili ya Kitanzania yaliyodumishwa katika kipindi cha ukoloni. Umahiri utakaoujenga utakuwezesha kuishi kwa kuzingatia maadili ya Kitanzania.
Fikiri
Maadili ya sasa ya jamii za Kitanzania.
Dhana ya Maadili Wakati wa Ukoloni
Dhana ya maadili wakati wa ukoloni inahusisha mifumo ya kutuawala, kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni ambayo ilietwa na wakoloni pamoja na ile iliyokuwepo kabla ya ujio wa wakoloni katika jamii za Kitanzania. Kwa kiasi kikubwa, Waafrika waliendelea kuziishi na kuzifuata mila na desturi zao, ingawa pia waliyapokea maadili mapya kama vile imani za kiroho, mifumo ya kutuawala na tamaduni za kigeni.
Kanuni za kikoloni zilisistitza uwajibikaji wa kila mtu, umiliki binafsi wa mali na heshima kulingana na nafasi ya mtu katika jamii. Hata hivyo, kanuni hizi kwa kiasi kikubwa zilikinzana na maadili ya Kitanzania yaliyokuwapo kabla ya ujio wa wakoloni. Hii ni kwa sababu jamii nyingi ziliamini katika uwajibikaji wa pamoja, umiliki wa mali kwa pamoja na heshima kwa wote bila kujali nafasi ya mtu katika jamii.
Kwa ujumla, maadili ya jamii za Kitanzania kabla ya ujio wa ukoloni katika jamii nyingi yaliongozwa na mfumo wa usawa.
Kazi ya Kufanya 2.1
Umealikwa kuwakilisha shule yako katika semina kuhusu mada isemayo "Vijana na Maadili". Andaa muhtasari utakaoutumia kuwasilisha mawazo yako kwa kutumia dondoo ziftatazo:
- Umuhimu wa maadili katika jamii; na
- Nafasi ya vijana katika kuyaenzi na kuyaendeleza maadili katika jamii.
Maadili ya Jamii za Kitanzania Wakati Ukoloni Unaingia
Katika jamii za Kitanzania, misingi ya maadili ilijengwa juu ya umoja, ushirikiano na mshikamano miongoni mwa wanajamii. Vilevile, utunzaji wa mazingira, heshima kwa wazee na viongozi na utunzaji na ubezi wa familia na jamaa vilikuwa ni sehemu muhimu ya maadili hayo. Aidha, nidhamu, uaminifu na utii kwa mila, miko na desturi za jamii zilikuwa nguzo kuu za maadili. Hata wakati wa ukoloni, misingi hii liendelea kudumishwa kwa kiasi kikubwa na jamii za Kitanzania licha ya changamoto zilizokuwepo.
Ukoloni ulipoingia katika jamii za Kitanzania mwishoni mwa karne ya 19, mfumo wa maadili ulokuwepo, ambao ulilenga kujenga mshikamano wa kijamii, kuheshimu tamaduni na kuishi kwa amani na utulivu. Mfumo huu ulijikita katika mila na desturi zilizorithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine, ukizingatia ushirikiano, utu, haki na heshima.
Zoezi la 2.1
- Bainisha misingi mikuu ya maadili ya jamii za Kitanzania wakati ukoloni unaingia.
- Eleza umuhimu wa kujifunza maadili ya jamii za Kitanzania ya wakati uliopita.
- Linganisha mfumo wa maadili wa jamii za Kitanzania kabla na baada ya ukoloni.
Mila na Desturi
Wakati wa kuingia kwa ukoloni, jamii za Kitanzania zilikuwa na mifumo thabiti ya maadili iliyoongozwa na kanuni, miiko, mila na desturi zao. Maadili kama vile uvumilivu, ukarimu, heshima kwa wazee na mamlaka, uadilifu, kujitolea, usawa na uwajibikaji yalikuwa sehemu muhimu ya maisha ya kila siku.
Kila jamii ilikuwa na taratibu zake za kimaadili ambazo zilisimamiwa na viongozi wa jadi pamoja na wazee wa ukoo. Vilevile, jamii za Kitanzania zilikuwa na utajiri mkubwa wa mila, desturi, kanuni, miiko na utaratibu uliorithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine.
Kundi la wazee wa ukoo liliheshimiwa sana na lilitegemewa katika kufanya uamuzi, ushauri, kupitisha ujuzi wa kitamaduni na kudumisha umoja wa familia. Wazee walikuwa na wajibu wa kurithisha mila na desturi kwa kizazi kijacho.
Dini za Jadi
Wakati ukoloni ulipoingia, dini za jadi zilikuwa na nafasi muhimu katika kuunda maadili ya jamii. Watu waliamini katika nguvu za asili, mizimu na miungu. Imani hizi ziliathiri na kukuza imani za watu na jinsi watu walivyoheshimu mazingira, walivyotekeleza shughuli za kilimo na walivyoishi kwa maelewano.
Maadili ya dini za jadi yalisisitiza ushirikiano, upendo, heshima, umoja kwa wanajamii, pamoja na kudumisha, kukuza na kufuata mila na desturi zilizorithiwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine.
Utawala wa Jadi
Wakati ukoloni ulipoingia, jamii za Kitanzania zilikuwa zikiongozwa na mifumo ya jadi iliyotofautiana baina ya kabila moja na lingine. Mifumo hii mara nyingi ilijikita katika kufanya uamuzi kijamii, ambapo majukumu ya uongozi yalitekelezwa na machifu, wazee, au mabaraza ya wazee.
Uamuzi wa viongozi hawa uliheshimiwa na wanajamii wote kutokana na hekima na uwezo wao wa kudumisha maelewano ndani ya jamii. Uongozi huo ulifanya uamuzi kwa faida ya jamii nzima na si kwa masilahi ya watu wachache.
Athari za Mfumo wa Ukoloni katika Maadili ya Kitanzania
Athari za Kijamii
Elimu: Kabla ya ukoloni, elimu katika jamii za Kitanzania ilitolewa kulingana na mazingira yao na ilijikita katika mila na desturi. Kulikuwa na mfumo rasmi wa utoaji elimu katika kila jamii, ambapo elimu hiyo ilitolewa wakati wote na kwa vitendo.
Mamlaka za kikoloni zilianzisha mifumo rasmi ya elimu iliyofuata mfumo wa elimu na maadili ya kimagharibi ya Ulaya. Shule za wamisionari zilifundisha masomo yanayohusu maadili ya kwao, huku mara nyingi zikikataa na kupinga mila, tamaduni na desturi za Kitanzania kuendelea kutumika miongoni mwa wanajamii.
Afya: Kabla ya ujio wa wakoloni, jamii za Kitanzania zilikuwa na mifumo mbalimbali ya utoaji huduma za afya, kulingana na tamaduni na mila za jamii iliyohusika. Kulikuwa na matumizi ya dawa za asili zilizotokana na mimea na vifaa vingine.
Ujio wa wakoloni ulileta mabadiliko makubwa katika mfumo wa afya, kwani walianzisha hospitali na vituo vya afya katika maeneo mbalimbali nchini kwa kutumia mtindo na mfumo wa Ulaya magharibi. Wakoloni walibeza na kudunisha mfumo wa tiba za asili kwa kutumia mbinu mbalimbali.
Athari za Kintamaduni
Dini za Jadi: Kabla ya kuja kwa dini za kigeni kama Ukristo na Uislamu, jamii za Kitanzania zilikuwa na imani za kiasili zilizokita mizizi katika utamaduni wa jamii iliyohusika.
Ujio wa ukoloni nchini uliathiri na kuleta mifumo mipya ya imani na dini, ambayo iliendana na utamaduni wa Ulaya Magharibi. Kwa mfano, wamisionari wa Kikristo walileta mafundisho mapya yenye mila, desturi na maadili mapya, huku wakilenga kubadilisha imani za jamii za Kitanzania.
Lugha: Kabla ya ukoloni, jamii za Kitanzania zilizungumza lugha za kiasili kama vile Kimasai, Kisukuma, Kichaga, Kizigua, Kizaramo, Kidigo, Kimwera, Kiumbatu na nyinginezo nyingi. Lugha hizi hazikuwa tu njia za mawasiliano, bali pia zilibeba utamaduni, utambulisho, mila, desturi, miko na kumbukumbu katika jamii iliyohusika.
Hata hivyo, mifumo ya elimu ya kikoloni illeta mabadiliko makubwa kwenye lugha za asili. Lugha kama Kiingereza kilianza kutumika kama lugha ya kufundishia shuleni, hali iliyosababisha kupungua kwa matumizi ya lugha za asili.
Zoezi la 2.3
- Bainisha athari zingine zilizoletwa na Ukristo nchini Tanzania.
- Linganisha mfumo wa elimu ya jadi na mfumo wa elimu ya sasa.
- Eleza mchango wa dini za jadi katika kulinda na kudumisha maadili ya Kitanzania.
- Fafanua umuhimu wa tiba za asili katika mazingira ya sasa ya Kitanzania.
Maadili ya Kitanzania Yaliyodumishwa Wakati wa Ukoloni
Maadili ya jamii za Kitanzania yaliendelea kudumishwa hata wakati wa ukoloni. Ingawa kulikuwa na jitihada kadhaa za kubadilisha maadili hayo kutokana na ushawishi wa wakoloni, bado maadili yaliendelea kuwa nguzo muhimu katika jamii.
Umoja na Ushirikiano: Dhana ya maisha ya jumuiya na uwajibikaji wa pamoja ilikuwa tunu kuu katika jamii nyingi za Kitanzania. Kwa mfano, miongoni mwa Wachaga wa Kilimanjaro, kilimo cha jumuiya na kazi za pamoja zilikuwa na umuhimu mkubwa.
Heshima kwa Wazee: Licha ya utawala wa kikoloni, jamii za Kitanzania ziliendelea kuzingatia kanuni za kiutamaduni zilizosisitiza heshima kwa wazee. Kwa mfano, jamii za Wazaramo wa eneo la pwani ziliendelea kushikilia maadili haya wakati wa ukoloni, ambapo wazee walitumika kutoa ushauri na kufanya uamuzi.
Ukarimu: Jamii za Kitanzania zilijulikana kwa ukarimu wao na thamani hii iliendelezwa hata wakati wa ukoloni. Jamii hizi ziliamini katika umuhimu wa kuwatendea wageni kwa heshima na ukarimu.
Utii kwa Mamlaka: Wakati wa utawala wa kikoloni, heshima kwa uongozi wa ndani na muundo ya kimila iliendelea kudumishwa. Heshima hii ilienea pia kwa watawala wa kikoloni, ingawa mara nyingi iliambatana na upinzani.
Kazi ya Kufanya 2.5
Fanya utafiti katika jamii unamoishi na bainisha maadili ya jamii za Kitanzania yaliyokuwepo wakati wa ukoloni ambayo bado yanaenziwa hadi wakati wa sasa.
Zoezi la Marudio
- Eleza dhana ya "maadili" katika utamaduni wa Mtanzania.
- Jadili nafasi ya vijana katika kukuza maadili kwa jamii ya Kitanzania.
- Eleza jinsi sera za kikoloni zilivyochangia katika mabadiliko ya maadili ya jamii za Kitanzania.
- Eleza athari za dini za kigeni katika mila na desturi za jamii za Kitanzania.
- Nini athari za mfumo wa elimu ya kikoloni katika maadili ya Kitanzania.
- Eleza matokeo ya muda mrefu ya ukoloni kwa maadili ya jamii ya Kitanzania.
- Fafanua mbinu mbalimbali zilizotumiwa na jamii za Kitanzania kupinga mifumo iliyokuwa inaathiri maadili yao wakati wa ukoloni.
Sura ya Tatu
Mapambano ya Awali Dhidi ya Uvamizi wa Kikoloni
Utangulizi
Jamii za Kitanzania zilitumia mbinu na njia mbalimbali kuukataa na kuupinga uvamizi wa kikoloni. Katika sura hii, utajifunza kuhusu dhana ya uvamizi wa kikoloni na sababu za kupinga uvamizi wa kikoloni. Pia, utajifunza mbinu na njia zilizotumika katika kuupinga uvamizi wa kikoloni. Umahiri utakaoujenga utakusaidia kuenzi, kuthamini na kuendeleza harakati za ukombozi dhidi ya unyonyaji na ukandamizaji wa aina mbalimbali katika jamii.
Fikiri
Mapambano ya jamii za Kitanzania dhidi ya uvamizi wa kikoloni.
Dhana ya Uvamizi wa Kikoloni
Uvamizi wa kikoloni ni kitendo cha nchi moja kuingia katika nchi nyingine kwa lengo la kuanzisha utawala wake kisiasa, kiuchumi na kijamii. Mara nyingi, uvamizi huu hutekelezwa kwa kutumia nguvu za kijeshi. Uanzishwaji wa utawala wa kikoloni hutegemea kushindwa kwa nchi inayovamiwa kujilinda au kuzuia uvamizi huo.
Uvamizi wa kikoloni nchini Tanzania (Tanganyika na Zanzibar) ulipingwa vikali kwa sababu jamii za Kitanzania zilifahamu kwamba kuruhusu wakoloni kuvamia kungesababisha kupoteza uhuru wao.
Kwa sababu za kizalendo na kupenda jamii zao, viongozi wengi wa jamii za Kitanzania waliongoza mapambano dhidi ya uvamizi huo tangu miaka ya 1880 na mapambano hayo yaliendelea hata baada ya ukoloni kuanzishwa nchini Tanganyika. Wananchi walipinga na kuonesha wazi hisia zao za kutokubali dhuluma na unyanyasaji kutoka kwa wakoloni, hali iliyojitokeza karibu katika kila sehemu ya Tanzania.
Mapambano ya awali dhidi ya wakoloni yalihusisha jamii moja moja, jambo ambalo linamaanisha kuwa, hatua za mwanzo za kuupinga uvamizi wa kikoloni hazikuhusisha nguvu za pamoja za jamii mbalimbali za Kitanzania au taifa moja la Tanzania.
Kazi ya Kufanya 3.1
Soma matini kutoka vyanzo mbalimbali na ubainishe tofauti ya uvamizi uliokuwepo kati ya Afrika Mashariki ya Kijerumani (Tanganyika) na Zanzibar.
Kazi ya Kufanya 3.2
Kwa kutumia taarifa kutoka vyanzo mbalimbali fanya uchunguzi kuhusu Karl Peters alivyoingia mikataba ya kilaghai. Andika insha yenye maneno mia tatu (300) ukiwashauri viongozi wa kizazi cha sasa kipi cha kujifunza kutokana na mikataba ya Karl Peters.
Sababu za Koupinga Uvamizi wa Kikoloni na Maadili Yake
Utawala wa kikoloni nchini Tanzania ulisababisha kupotea kwa uhuru, kudunishwa na kuharibiwa kwa maadili ya jamii. Wakoloni walidhihaki mila na desturi ambazo zilikuwa msingi wa maadili ya jamii. Hali hii iliwachochea wananchi, chini ya uongozi wa viongozi wao hodari na shupavu wa jadi, koupinga utawala wa kigeni ili kulinda uhuru, utamaduni na maadili yao.
Aidha, wananchi walinyonywa kwa kulazimishwa kufanya kazi za vibarua na kulipwa ujira mdogo katika mashamba ya nkonge, pamba, chai, tumbaku na pareto. Wakulima, wakiwa chini ya usimamizi mkali wa majumbe na wanyapara, walidhalilishwa kwa kuchapwa viboko.
Zaidi ya hayo, mfumo mpya wa kodi ulioanzishwa na wakoloni uliwalazimisha wananchi kulipa kodi ya kichwa na kodi nyingine kwa pesa tasilimu. Jambo hili liliwakera sana kwa kuwa hawakuwa na pesa, hivyo walilazimika kuuza mifugo yao, kufanya kazi za vibarua kwa wakoloni na walowezi au kulima mazao ya biashara ili kupata pesa za kulipa kodi.
Wakoloni walitumia adhabu za kikatili kama kuwanyonga viongozi wa jamii za Kitanzania walioppinga utawala na maadili yao. Wananchi pia waliteswa na kudhalilishwa hadharani kwa kuchapwa viboko waliposhindwa kulipa kodi au walipotenda makosa mengine dhidi ya utawala wa kikoloni, jambo lilioshusha heshima, ushujaa na utu wao ambao ulikuwa umejengwa kwa muda mrefu na jamii zao za asili.
Kazi ya Kufanya 3.3
Fanya utafiti mdogo, kisha andika taarifa kuhusu jinsi uvamizi wa kikoloni ulivyosababisha mmomonyoko wa maadili katika jamii za Kitanzania.
Upinzani Dhidi ya Uvamizi wa Kikoloni Katika Jamii za Kitanzania
Karibu jamii zote za Kitanzania ziliupinga uvamizi wa kikoloni kwa sababu hakuna jamii iliyopenda kuupoteza uhuru na utamaduni wake kwa wageni. Jinsi jamii hizi zilivyoupinga uvamizi huo, au njia gani walizozitumia zilitegemea uwezo wa kivita, kiuchumi, mazingira na uongozi bora na imara. Kwa hiyo, kuna jamii zilizoupinga ukoloni kwa kupigana vita, zingine kwa kujisalimisha na nyingine kwa kuungana na wavamizi.
Njia ya Kupambana kwa Vita
Njia ya vita ilikuwa maarufu zaidi kati ya jamii za Kitanzania, kwani jamii nyingi hazikuwa tayari kuupoteza uhuru wao na hivyo ziliupinga waziwazi uvamizi huo kwa kutumia vita. Jamii hizi nyingi zilikuwa na uongozi shupavu, zilimiliki silaha, zilikuwa na uwezo wa kiuchumi na nyingi pia zilikuwa chini ya dola zenye nguvu.
Mapambano dhidi ya uvamizi yalihusisha jamii moja moja au jamii nyingi kwa pamoja. Kwa mfano, mapambano ya mwanzo dhidi ya uvamizi wa kikoloni na maadili yake yalihusisha jamii moja moja na siyo makabila mengi au nchi nzima.
Mapambano ya Wanyamwezi
Harakati za kupinga uvamizi wa kikoloni magharibi mwa Afrika Mashariki ya Kijerumani, ziliongozwa na Mtemi wa Wanyamwezi aliyejulikana kama Isike au Mwana Kiyungi kuanzia mwaka 1886 hadi 1891. Mtemi Isike alipinga vikali uvamizi wa Wajerumani katika himaya yake baada ya maeneo yake ya kintawala kuporwa.
Ili kulinda uhuru na maadili ya jamii ya Wanyamwezi, Mtemi Isike aliwaongoza kwa ushupavu askari wake kupambana na majeshi ya Wajerumani. Zaidi ya askari 1000 wa jeshi la Wajerumani walipambana vikali na askari wa Isike. Hata hivyo, ngome ya Mtemi Isike ilivunjwa na majeshi ya kivamizi ya Wajerumani. Isike alipoelemewa, aliona ni bora ajiue kuliko kukamatwa na Wajerumani, hivyo alijilipua kwa baruti pamoja na familia yake mnamo mwaka 1893.
Mapambano ya Jamii za Watu wa Pwani
Mapambano ya awali dhidi ya uvamizi wa Kijerumani katika ukanda wa pwani ya Afrika Mashariki ya Kijerumani (sasa Tanzania) yaliongozwa na wafanyabiashara mashuhuri Abushiri bin Salim al-Harthi wa Pangani na Bwana Heri bin Juma wa Uzigua.
Kielelezo 3.1: Abushiri bin Salim
Abushiri bin Salim
Mwaka 1889, Abushiri bin Salim aliwaongoza wananchi wa pwani katika maeneo ya Pangani kupigana na Wajerumani na kufanikiwa kuwaondoa katika baadhi ya maeneo ya pwani. Kutokana na upinzani mkali alioutoa kwa majeshi ya Kijerumani, Wajerumani waliomba msaada kutoka kwa majeshi ya Uingereza.
Bwana Heri bin Juma aliwaongoza Wazigua wa maeneo ya Saadani dhidi ya uvamizi wa Wajerumani. Ingawa baadaye alishindwa, aliendesha mapambano makali ambayo yalionesha jinsi wananchi walivyokuwa hawako tayari kunyanyaswa na kunyonywa na Wajerumani.
Mapambano ya Wahehe
Jamii ya Wahehe chini ya uongozi wa Mtwa Mkwawa, ilipinga vikali uvamizi wa Wajerumani kati ya mwaka 1891 na 1898 kwa njia ya vita. Kabla ya uvamizi huo, Wahehe walikuwa wamejiimarisha kibiashara kwa kudhibiti maeneo mengi.
Kielelezo 3.2: Mtwa Mkwawa
Mtwa Mkwawa
Sababu kubwa ya mapambano ya Wahehe dhidi ya Wajerumani ilikuwa kuyalinda maadili, uhuru na masilahi yao, hasa ya kiuchumi. Mapambano ya kwanza ya kijeshi kati ya Wahehe na Wajerumani yalifanyika mwaka 1891 katika eneo la Lugalo. Katika mapigano hayo, wapiganaji wa Kihehe waliwashinda Wajerumani na askari 300 wa Kijerumani pamoja na kiongozi wao waliuawa.
Mwaka 1898, Mtwa Mkwawa aliamua kujiua badala ya kukamatwa na Wajerumani. Kifo cha namna hii kilikuwa ushujaa wa aina yake, kwani Mkwawa aliona ni fedheha kwa shujaa kukamatwa, kunyanyaswa na kuuawa kikatili kwa kunyongwa na wavamizi.
Mapambano ya Wayao
Mapambano ya kupinga uvamizi wa Wajerumani upande wa kabila la Wayao yaliongozwa na kiongozi wao jasiri na shupavu, Mwene Machemba. Mwene Machemba alishinda karibu mapigano yote aliyoyaongoza dhidi ya Wajerumani.
- Mwene Machemba katika barua kwa Wajerumani
Kielelezo 3.4: Mwene Machemba
Mwene Machemba
Kazi ya Kufanya 3.4
Mapambano ya kupinga uvamizi wa kikoloni hayakuwa lelemama. Machifu na Waterni waliyapoteza maisha yao wakitetea maadili na ardhi yao isivamiwe na wageni. Soma matini kutoka vyanzo mbalimbali na uandike taarifa kuhusu viongozi walionyongwa kwa koupinga uvamizi wa kikoloni.
Changamoto Zilizokabili Mapambano Dhidi ya Uvamizi wa Kikoloni
Wananchi walijaribu kupambana na kupinga ukoloni, lakini wakoloni waliwazidi nguvu na kuwashinda. Zipo sababu nyingi zilizowafanya wananchi kushindwa katika mapambano hayo.
Ukosefu wa Umoja Miongoni mwa Jamii za Kitanzania
Kama ilivyoonekana, mapambano dhidi ya ukoloni yalifanywa kati ya wakoloni na jamii moja moja za Kitanzania. Hii inamaanisha kuwa, katika kipindi cha ukoloni, jamii za Kitanzania zilishindwa kwa sababu zilikosa umoja na hazikushirikiana kupambana na wakoloni.
Matumizi ya Silaha Duni Dhidi ya Silaha Bora za Wajerumani
Katika sehemu kubwa ya Tanzania, wananchi walioshiriki katika mapambano hawakufanikiva kuuangusha utawala wa kikoloni kwa sababu Wajerumani walitumia silaha bora zaidi kuliko zile zilizotumiwa na wananchi. Kwa mfano, Wajerumani walitumia mizinga na bunduki, wakati wananchi walitumia pinde, mishale, ngao, mawe, marungu na majambia.
Usaliti
Baadhi ya viongozi wa jadi waligeuka kuwa vibaraka wa serikali ya kikoloni. Katika maeneo mengi, baadhi ya jamii za Kitanzania ziliungana na Wajerumani kupigana na jamii zingine za Kitanzania. Hii ilisababisha jamii nyingi kushindwa vita, kwani jamii jirani zilizoungana na Wajerumani ziliwasaidia kufichua udhaifu na nguvu za jamii hizo na hivyo kurahisisha ushindi kwa Wajerumani.
Kazi ya Kufanya 3.6
Fanya utafiti kupitia vyanzo mbalimbali vya taarifa ili kubaini sababu nyingine zilizosababisha Watanzania kushindwa katika vita dhidi ya uvamizi wa kikoloni.
Matokeo ya Kupinga Uvamizi wa Kikoloni
Ni muhimu kukumbuka kuwa jamii za Kitanzania zilipambana vikali koupinga ukoloni. Kutokana na matumizi ya silaha duni za jadi, wakoloni walifanikiwa kuzishinda na kuendelea kuzitawala. Katika kipindi chote cha vita, wananchi walijitoa kwa hali na mali, wakiongozwa na viongozi wa jadi waliotetea uhuru, haki, masilahi na utu wao.
Matokeo ya mapambano hayo yalikuwa kama ifuatavyo:
- Shughuli za uzalishaji mali zilisimama: Kipindi chote cha vita, badala ya kuzalisha, muda mwingi ulitumika katika kujipanga kivita na kupigana. Hali hii ilisababisha upungufu wa chakula na kuleta njaa kubwa.
- Kutumikishwa kwa nguvu kazi ya vijana: Wanaume, hasa vijana wenye nguvu, walisafirishwa mbali na makazi yao na kutumikishwa katika mashamba ya walowezi.
- Vifo kutokana na wanyama pori: Athari nyingine ya vita ilikuwa vifo vilivyosababishwa na wanyama pori. Wakati wa vita, wapiganaji walitumia muda mwingi msituni.
- Hofu miongoni mwa Watanzania: Vita vilisababisha kujengeka kwa hofu miongoni mwa Watanzania. Kutokana na kushindwa kwa mapambano, watu wengi walipata hofu ya kupigana tena na Wazungu.
- Mateso na vifo vingi: Vita vya kupinga uvamizi wa wakoloni vilisababisha maelfu ya vifo katika mapambano, kukamatwa kwa mateka, kunyongwa na vifo vilivyotokana na njaa wakati na baada ya vita.
- Mwamko mpya wa harakati za uhuru: Ingawa jamii za Kitanzania zilishindwa katika mapambano ya awali dhidi ya uvamizi wa kikoloni, mapambano hayo yaliacha alama muhimu katika historia.
- Kumbukumbu muhimu katika historia ya Tanzania: Hapana shaka kwamba vita vya kupinga ukoloni ni kumbukumbu muhimu katika historia ya Tanzania inayostahili kuheshimiwa na yeyote anayethamini utu, uhuru, haki, heshima na usawa.
Zoezi la Marudio
- Tofautisha kati ya maadili ya kikoloni na maadili ya jamii za Kitanzania wakati ukoloni unaingia.
- Eleza sababu za kushindwa kwa mapambano ya awali ya jamii za Kitanzania dhidi ya uvamizi wa kikoloni.
- Eleza jinsi viongozi wa sasa wanapaswa kutetea masilahi ya wananchi kwa ujasiri na uzalendo.
- Bainisha vitendo vya kijasiri vilivyooneshwa na viongozi wa jamii za Kitanzania walioongoza mapambano ya awali dhidi ya uvamizi wa kikoloni.
- Je, unafikiri ni namna gani mbinu ya jadi ya kivita iliyotumiwa na Kinjeketile ilisaidia katika kupinga uvamizi wa Wajerumani?
- Ni funzo gani viongozi wa sasa wanaweza kujifunza kutoka kwa jamii za Kitanzania zilizopinga uvamizi wa kikoloni?
Sura ya Nne
Harakati za Kudai Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar
Utangulizi
Harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar ziliendana na juhudi mbalimbali za kisiasa na kijamii zilizolenga kukomesha utawala wa kikoloni. Katika sura hii, utajifunza kuhusu dhana ya uhuru na harakati za kudai uhuru, pamoja na misingi na mbinu zilizotumika katika kupigania uhuru wa Tanganyika na Zanzibar. Pia, utajifunza mchango wa harakati hizo katika kuupinga utawala wa kikoloni, kuyatunza maadili ya Kitanzania na kuujenga uzalendo. Umahiri utakaoupata utakuwezesha kuthamini juhudi za wapigania uhuru wa Tanganyika na Zanzibar na pia kuuheshimu na kuuenzi uhuru wetu.
Fikiri
Harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar.
Dhana ya Uhuru na Harakati za Kudai Uhuru
Neno "uhuru" linaweza kufafanuliwa kwa namna mbalimbali. Uhuru ni hali ya mtu au nchi kuamua na kufanya mambo yake bila kuingiliwa na mtu au taifa lolote, iwe kiuchumi, kisiasa, kijamii au kiutamaduni. Katika muktadha huu, uhuru ni hali ya nchi kujikomboa kutoka kwenye ukoloni wa mataifa ya kibepari.
Harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar ni mchakato au juhudi za watu wa nchi hizo kutafuta uhuru kutoka kwa serikali za kikoloni. Pia, ni hatua zilizochukuliwa na wananchi wa Tanganyika na Zanzibar hadi kufanikisha kupata uhuru wao.
Tanganyika ilitawaliwa na wakoloni wa Kijerumani kuanzia mwaka 1885 hadi 1918. Baada ya Vita ya Kwanza vya Dunia, Tanganyika ilitawaliwa na Waingereza hadi ilipopata uhuru wake tarehe 9 Desemba, 1961.
Zanzibar ilikuwa chini ya utawala wa Kisultani kutoka Oman kuanzia mwaka 1840 hadi 1890, kisha ikatawaliwa na Waingereza kuanzia mwaka 1890 hadi 1963. Baada ya harakati za kutafuta uhuru, Waingereza walikabidhi uhuru wa Zanzibar kwa vyama vya ZNP na ZPPP chini ya Sultani Jamshid bin Abdullah Al Said tarehe 10 Desemba, 1963.
Hata hivyo, harakati za ukombozi wa Waafrika walio wengi zilifanikiva kupitia Mapinduzi Matukufu ya tarehe 12 Januari, 1964. Hivyo, ilikuwa ni jukumu muhimu kwa wananchi wa Tanganyika na Zanzibar kuanzisha harakati za kuudai uhuru na kujikomboa kutoka katika ukoloni wa Kisultani na Kiingereza.
Misingi ya Kudai Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar
Harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar zilianza mara tu baada ya kuanzishwa kwa serikali za kikoloni. Watanzania wengi hawakupendezwa na tawala za kikoloni na hivyo wakaanzisha mapambano na harakati za kupinga tawala hizo. Zipo sababu kadhaa zilizowafanya Watanzania kuanzisha harakati za kudai uhuru wao.
Unyonyaji wa Mali na Rasilimali
Mfumo wa kikoloni ulikuwa wa kinyanyasaji na kinyonyaji. Watanzania walinyonywa katika nchi yao. Mathalani, walifanya kazi maeneo mbalimbali kama vile mashambani, migodini na sehemu nyingine za nchi bila kupata ujira unaostahili.
Pia, mfumo wa kikoloni uliwalazimisha wananchi kulima mazao yaliyoletwa na wakoloni kwa ajili ya viwanda vyao vilivyopo Ulaya. Sera za kikoloni zilizokuwa za kinyonyaji zilisababisha Watanzania kuachana na malengo ya kufanya kazi kwa ajili ya kuzalisha mazao yaliyoletwa na wakoloni.
Sera za Kibaguzi
Katika kipindi cha ukoloni, sera mbalimbali za kibaguzi zilianzishwa kupitia huduma za jamii na ajira. Kwa mfano, wananchi walibaguliwa katika kupata huduma za kijamii kama vile; afya, elimu na makazi.
Wazungu, Waarabu na Waasia walipewa huduma bora wakati Waafrika wakipewa huduma duni au kutokupewa kabisa. Vilevile, kulikuwa na ubaguzi katika kupata ajira zenye hadhi. Kwa ujumla, Waafrika walipewa kazi za usaidizi na zile za ngazi ya chini sana zilizosababisha kulipwa ujira mdogo usioendana na uzito wa kazi walizokuwa wakifanya.
Ukandamizwaji wa Waafrika
Wakoloni walipofika walianza kupora ardhi nzuri ya uzalishaji mali kutoka kwa wenyeji. Hivyo, ili watu waweze kuishi, iliwalazimu kufanya kazi katika mashamba ya wakoloni kwa ujira mdogo na wakati mwingine bila malipo.
Pia, serikali za kikoloni ziliwatoza kodi wananchi kwa nguvu na kuwafanyisha kazi katika mashamba yao kwa ujira mdogo. Vilevile, katika maeneo mengine, Watanzania waliazimishwa kujenga miundombinu mbalimbali.
Kudhihakiwa kwa Mila na Desturi za Watanzania
Wakoloni kupitia Wamisionari walipiga marufuku mila na desturi za Kiafrika. Kwa mfano, majina ya Kiafrika yalionekana ni ya "kishenzi" na vilevile dini za jadi zilionekana ni za "kishenzi".
Baadhi ya vyakula, nguo, lugha na sanaa vilipigwa marufuku. Badala yake walitilia mkazo matumizi ya utamaduni wa kigeni. Dini za Ukristo na Uislamu zikawa ni alama ya ustaarabu kwa Waafrika waliozifuata imani hizi.
Kazi ya Kufanya 4.1
Soma matini kutoka vyanzo mbalimbali ikiwemo mitandao ili kubainisha misingi mingine ya kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar.
Mbinu Zilizotumika Kudai Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar
Kuna vipindi viwili muhimu vya harakati za wananchi katika kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar. Kipindi cha kwanza kilikuwa kati ya mwaka 1900 hadi 1944. Katika kipindi hicho, harakati ziliendeshwa na vikundi na vyama vya kijamii na kidini (hasa kwa upande wa Tanganyika) katika maeneo machache tu.
Kipindi cha pili cha harakati hizi kilikuwa kati ya mwaka 1945 na 1964, ambapo harakati za kudai uhuru zilikuwa na nguvu zaidi zikiendeshwa na vyama vya siasa. Katika kipindi hiki, harakati hizo zilisambaa nchi nzima kutokana na mabadiliko yaliyotokana na mchango wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia (1939 – 1945).
Harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar zilitumia mbinu mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kuanzisha jumuiya, vyama na taasisi za kijamii za Waafrika. Malengo ya kuanzishwa kwa jumuiya, vyama na taasisi hizo yalikuwa ni kutetea na kudai haki za wafanyakazi, wakulima na wafanyabiashara.
Vyama vya Ushirika na Wakulima
Chama cha ushirika ni muungano wa watu waliokubaliana kuendesha shughuli zao za kiuchumi kwa pamoja ili kuinua hali zao za maisha. Shughuli hizi ni kama vile kutafuta mahitaji yao ya chakula, elimu, uuzaji wa mazao yao na shughuli nyingine za uchumi zinazoweza kuendeshwa kwa pamoja.
Vyama vya wakulima vilianzishwa na wakulima wenyewe katika maeneo ambapo mazao ya biashara yalilimwa. Vyama hivi vilijulikana kama vyama vya ushirika katika sehemu mbalimbali za Tanganyika na Zanzibar.
Kielelezo 4.1: Clement George Kahama (kushoto) na Paul Bomani (kulia)
Clement George Kahama (kushoto) na Paul Bomani (kulia)
Baadhi ya malengo ya kuanzishwa kwa vyama hivi yalikuwa ni pamoja na kudai bei nzuri ya mazao yao, kupata masoko ya uhakika, kudai kupewa pembejeo na zana za kilimo, kupinga unyonyaji, kunyang'anywa ardhi na kutozwa kodi kubwa ya mazao yao.
Mfano wa vyama hivi vya wakulima ni: Bukoba Buhaya Union (1924), Kilimanjaro Native Planters Association (1925), Meru Citizens' Union (1930), Sukuma Union (1930), Chama cha Waluguru cha African Cotton Planters Association (1934), Nyakyusa Union (1937), Buhaya Farmers' Association (1937) na Pare Union (1949).
Vyama vya Wafanyakazi
Waafrika waliokuwa wameajiriwa katika viwanda, mashamba, bandari na sehemu nyingine walianzisha vyama vyao vya wafanyakazi kwa lengo la kulinda na kutetea masilahi yao ya kikazi. Malengo hayo yalijumuisha kudai kulipwa mishahara kwa wakati, ujira unaostahili na mazingira bora ya kazi.
Kielelezo 4.2: Rashid Mfaume Kawawa
Rashid Mfaume Kawawa
Mfano wa vyama hivyo ni Tanganyika Territory Civil Servants'Association (TTCSA), kilichoanzishwa na Martin Kayamba mwaka 1922 huko Tanga, ambacho mwaka 1924 kilifungua tawi lake mjini Dar es Salaam.
Pia, ndani ya kipindi hicho cha mwaka 1922 wafanyakazi wa serikali wa Dar es Salaam walianzisha Tanganyika African Government Servants Association (TAGSA). Vyama vingine vilivyoundwa ni pamoja na Association of Cooks and Washmen (1939), Dock Workers' Union (1937), Railway African Civil Service Union (1920) na Tanganyika Federation of Labour (1955) chini ya uongozi wa Rashid Mfaume Kawawa.
Vyama vya Siasa
Umoja wa Waafrika ulio itwa African Association (AA) uliundwa mwaka 1929 na mnamo mwaka 1948 ulipewa jina jipya la Tanganyika African Association (TAA). Mwaka 1954, chama hiki kilibadilishwa jina tena na kuwa chama rasmi cha siasa kwa jina la TANU.
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
Alikuwa kiongozi mkuu wa harakati za uhuru wa Tanganyika na mwanzilishi wa TANU. Alikuwa na uwezo wa kuwaunganisha Watanzania wa makabila yote katika harakati za ukombozi.
Sheikh Abeid Amani Karume
Alikuwa kiongozi mkuu wa Zanzibar na mwanzilishi wa ASP. Aliongoza harakati za ukombozi Zanzibar na baadaye kuwa Rais wa kwanza wa Zanzibar baada ya Mapinduzi.
Chama cha TANU kilikuwa na malengo mengi na baadhi ya malengo hayo yalikuwa ni pamoja na kuwaunganisha wananchi wa Tanganyika na kuwaongoza katika mapambano ya kupigania uhuru wa nchi yao, kutoa tafsiri mpya ya ukombozi, kuweka juhudi na fikra mpya za mapambano kwa misingi ya kifalsafa, pamoja na kudai haki ya kuwa na wawakilishi wa kidemokrasia katika vyombo vya kutunga sheria.
Mbali na chama cha TANU, kulikuwa na vyama vingine vya kisiasa wakati wa harakati za kupigania uhuru. Mfano wa vyama hivyo ni United Tanganyika Party (UTP) kilichoanzishwa mwaka 1956, ambacho kiliungwa mkono na Wazungu, Waasia na baadhi ya Waafrika, hasa machifu.
Kwa upande wa Zanzibar, vyama vilivyojitokeza kudai uhuru ni pamoja na Zanzibar Nationalist Party (ZNP) kilichoanzishwa mwaka 1955, Afro-Shirazi Party (ASP) kilichoanzishwa mwaka 1957 na Zanzibar and Pemba People's Party (ZPPP) lilioundwa mwaka 1959.
Kazi ya Kufanya 4.2
Chagua chama kimojawapo cha ushirika au wafanyakazi kilichoshiriki harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar, kisha soma matini mbalimbali kupitia mtandao kuhusu chama hicho na andika maelezo yenye kurasa 2 kuhusu historia na mchango wake katika harakati za kudai uhuru.
Vyombo vya Habari na Sanaa katika Harakati za Uhuru
Kuanzishwa kwa vyombo vya habari katika Tanganyika na Zanzibar kuliongeza na kuimarisha harakati za Waafrika katika kupigania uhuru wao. Kabla ya kuanzishwa kwa vyombo hivi vya Waafrika, kulikuwepo vyombo vya habari vilivyokuwa vimeanzishwa na serikali ya kikoloni.
Kutokana na changamoto hii, Waafrika wakaona kuwa kuna umuhimu wa kuunda na kuanzisha vyombo vya habari vyao wenyewe. Mfano wa vyombo hivyo ni gazeti la Kwetu, liliioanzishwa na jumuiya ya African Association (AA) mwaka 1937 na Sauti ya TANU, ambalo lilihaririwa na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mwaka 1957.
Kielelezo 4.4: Ukurasa wa mbele wa gazeti la Sauti ya TANU
Ukurasa wa mbele wa gazeti la Sauti ya TANU
Kwa upande wa Zanzibar, kulikuwepo na vyombo vya habari kama magazeti na majarida mbalimbali, kwa mfano, gazeti la Sauti ya Zanzibar (1949), gazeti la Samachar liliioandikwa na Bwana Moro bin Abu Rehan, jarida la African Events na Alfalaq (1929) liliioandikwa na Ahmed Yahya Aldarda.
Vyombo vya habari vya Waafrika vilienga kuamsha ari ya uzalendo kwa Watanganyika na Wazanzibari ili kuwaunganisha katika kudai uhuru wao. Viliikuwa na jukumu la kutoa elimu ya uzalendo na kuwaelimisha wananchi kuhusu sera na itikadi za vyama kama TANU na ASP.
Vikundi na Vyama vya Sanaa
Wakati wa utawala wa kikoloni, hakukuwa na nafasi ya kutosha kwa Watanganyika na Wazanzibari kusimama na kujieleza kwa uhuru kuhusu haki zao na harakati za ukombozi. Badala yake, mambo mengi ya harakati za Watanganyika na Wazanzibari kudai uhuru yalifanyika kwa siri kuhofia adhabu kutoka kwa wakoloni.
Viongozi na wanachama wa TANU na ASP waliamua kutumia sanaa na michezo kama mbinu mbadala. Sanaa ilitumika katika kukuza na kuendeleza harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar.
Kielelezo 4.5: Bibi Titi Mohamed akiwa jukwaani
Bibi Titi Mohamed akiwa jukwaani
Watanganyika walianzisha vikundi na vyama vya sanaa na michezo kama vile kikundi cha taarabu cha Jipisheni. Kikundi hicho baadaye kilipewa jina la Egyptian Music Club. Kikundi kingine cha taarabu kilikuwa ni Al-Watan.
Pamoja na taarabu kulikuwa vikundi vya lelemama ambavyo vilikuwa na udugu na vikundi vya taarabu vya Al-Watan au Egyptian. Vikundi vyote hivi vilitoa mchango mkubwa sana katika kuhamasisha watu kuiunga mkono TANU.
Waliounganisha na kuviongoza vyama hivi vya wanawake na harakati za kudai uhuru walikuwa Bibi Titi Mohamed na Bibi Hawa binti Maftah.
Kazi ya Kufanya 4.3
Soma matini kutoka vyanzo mbalimbali ikiwemo mitandao, kisha fafanua jinsi vikundi na vyama vya kidini vilivyochangia katika harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar.
Zoezi la Marudio
- Je, ni kwa namna gani mbinu ya kuanzisha vyama vya kiraia ilisaidia harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika na Zanzibar?
- Jadili nafasi ya vyombo vya habari katika harakati za kisiasa wakati wa sasa.
- Fafanua nafasi ya vijana katika kudumisha uhuru wa Tanganyika na Zanzibar.
- Eleza mchango wa vikundi na vyama vya kijamii na kidini katika kukukuza demokrasia wakati wa sasa.
- Pendekeza mikakati ya kudumisha uhuru wa Tanganyika na Zanzibar.
- Tofautisha mbinu zilizotumiwa na TANU na ASP katika kupigania uhuru.
- Eleza umuhimu wa ushirikiano wa kimataifa katika harakati za uhuru za Tanganyika na Zanzibar.
Sura ya Tano
Ujenzi wa Taifa Baada ya Ukoloni
Utangulizi
Baada ya kupata uhuru, nchi ya Tanganyika na baadaye Tanzania ilikabiliwa na changamoto kubwa ya kujenga taifa lenye misingi imara la kiuchumi, kisiasa na kijamii. Katika sura hii, utajifunza kuhusu dhana ya ujenzi wa taifa, mifumo iliyojengwa kati ya mwaka 1961 hadi 1966, mikakati ya ujenzi wa taifa na changamoto zilizokabili ujenzi huo. Umahiri utakaoujenga utakuwezesha kuchangia kwa ufanisi katika ujenzi wa taifa la Tanzania.
Fikiri
Juhudi za kujenga taifa baada ya ukoloni.
Dhana ya Ujenzi wa Taifa
Ujenzi wa taifa ni mchakato wa kuunda na kuimarisha utambulisho wa kitaifa, mfumo wa kisiasa, uchumi na jamii katika nchi huru baada ya ukoloni. Ni juhudi za kuwaunganisha wananchi wa makabila na tamaduni mbalimbali katika dhana moja ya utaifa, na kujenga jamii yenye misingi ya haki, usawa na maendeleo ya pamoja.
Baada ya kupata uhuru mwaka 1961, Tanganyika ilikabiliwa na changamoto nyingi za kijamii, kiuchumi na kisiasa. Mfumo wa kikoloni ulikuwa umeacha nyuma mgawanyo wa kikabila, uchumi uliotegemea uzalishaji wa malighafi tu, na jamii iliyogawanyika kimatabaka.
Ujenzi wa taifa ulihusisha:
- Kuunda utambulisho wa kitaifa uliounganisha Watanzania wote
- Kujenga mfumo wa kisiasa wa kidemokrasia
- Kuunda uchumi wa kujitegemea
- Kuharakisha maendeleo ya kijamii kama elimu na afya
- Kulinda uhuru na utu wa Watanzania
Mifumo Iliyojengwa Kati ya Mwaka 1961 hadi 1966
Mfumo wa Kisiasa
Baada ya uhuru, serikali ya kwanza ya Tanganyika chini ya Waziri Mkuu Julius K. Nyerere ilianzisha mfumo wa kisiasa uliokolea misingi ya uhuru, umoja na ustawi wa raia.
Kielelezo 5.1: Baraza la Kwanza la Mawaziri la Tanganyika mwaka 1961
Baraza la Kwanza la Mawaziri la Tanganyika mwaka 1961
Mafanikio Makuu ya Kisiasa
- Uundwaji wa Katiba ya kwanza ya Tanganyika (1962)
- Kuundwa kwa Jamhuri ya Tanganyika na Julius K. Nyerere kuwa Rais wa kwanza (1962)
- Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kuunda Tanzania (1964)
- Kuanzishwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya kuungana kwa TANU na ASP (1977)
Mfumo wa Kijeshi
Baada ya uhuru, jeshi la Tanganyika lilijengwa upya ili kulinda uhuru na utulivu wa nchi. Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) lilianzishwa mwaka 1963 kwa lengo la kujenga uraia mwema na kutoa mafunzo ya kijeshi kwa vijana.
Kielelezo 5.2: Brigedia Mirisho Sam Hagai Sarakikya
Brigedia Mirisho Sam Hagai Sarakikya
Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) lilianzishwa baada ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, na likawa ndio msingi wa ulinzi wa Tanzania.
Mfumo wa Kiuchumi
Serikali ya uhuru ilianzisha mifumo mipya ya kiuchumi ili kukabiliana na mirathi ya kikoloni ya uchumi wa kunyonywa. Mipango mikuu ilijumuisha:
- Mpango wa Maendeleo ya Kwanza (1964-1969): Kulenga kuinua uchumi wa nchi kupitia uwekezaji katika sekta muhimu kama kilimo, elimu na afya.
- Azimio la Arusha (1967): Lililenga kuweka misingi ya ujamaa na kujitegemea, na kukabiliana na ubaguzi na umasikini.
- Uundwaji wa Vyama vya Ushirika: Ili kuimarisha uchumi wa vijijini na kuwawezesha wakulima kushiriki kikamilifu katika uchumi.
Mfumo wa Kijamii
Serikali ya uhuru ilianzisha mabadiliko makubwa katika mfumo wa kijamii, hasa katika sekta ya elimu na afya:
Mafanikio ya Kijamii
- Kupanua upatikanaji wa elimu ya msingi kwa watoto wote
- Kuanzishwa kwa Elimu ya Siasa (1967) ili kukuza maadili ya ujamaa
- Uundwaji wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (1961) na vyuo vingine vya elimu ya juu
- Kupanua huduma za afya vijijini kupitia vituo vya afya
Mikakati ya Ujenzi wa Taifa
Ujamaa na Kujitegemea
Azimio la Arusha la mwaka 1967 liliweka misingi ya ujenzi wa taifa la Tanzania. Azimio hili lilihakikisha kuwa:
- Uchumi wa Tanzania ujengeke kwa misingi ya haki na usawa
- Rasilimali za nchi zitumike kwa manufaa ya wananchi wote
- Watanzania wote washiriki kikamilifu katika ujenzi wa taifa
- Maadili ya kujitolea, umoja na ushirikiano yatafuatiwe
Mikakati mikuu ya kiuchumi ilijumuisha uundwaji wa vijiji vya ujamaa, uanzishwaji wa mashirika ya umma na kuweka mipaka ya umiliki wa mali kwa viongozi.
Elimu ya Siasa
Elimu ya siasa ilianzishwa kwa lengo la kukuza maadili ya ujamaa na kuelimisha wananchi kuhusu haki na wajibu wao katika jamii. Ilikuwa ni sehemu muhimu ya kujenga utambulisho wa kitaifa na kupanua ushiriki wa raia katika masuala ya kisiasa.
Mwalimu Nyerere alisisitiza kuwa "Elimu ya siasa ni muhimu kwa raia wa Tanzania kama vile hewa ya kupumua."
Utamaduni na Sanaa
Serikali ilitambua umuhimu wa utamaduni na sanaa katika kujenga taifa. Ilianzisha taasisi kama:
- Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA): Ili kukuza na kustandardisha matumizi ya Kiswahili
- Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA): Ili kuendeleza na kuhifadhi sanaa za asili
- Baraza la Michezo la Taifa (BMT): Ili kukuza michezo kama chombo cha umoja wa kitaifa
Kielelezo 5.3: Nuta Jazz Band
Nuta Jazz Band - Mojawapo ya vikundi vya muziki vilivyokuwa chombo muhimu cha ujenzi wa taifa
Ushirikiano wa Kimataifa
Tanzania ilichukua nafasi muhimu katika shirika la siasa la kimataifa, ikiwa ni mwanachama mwanzilishi wa:
- Shirikisho la Afrika (sasa Umoja wa Afrika)
- Jumuiya ya Madola
- Harakati zisizo na Mpangilio (Non-Aligned Movement)
Ushirikiano huu ulisaidia Tanzania kupata usaidizi wa kiuchumi na kiteknolojia na pia kuchukua nafasi muhimu katika mapambano dhidi ya ukoloni barani Afrika.
Changamoto za Ujenzi wa Taifa
Licha ya juhudi nzuri za ujenzi wa taifa, Tanzania ilikabiliana na changamoto nyingi baada ya uhuru:
Changamoto za Kiuchumi
- Uchumi uliobaki kuwa unategemea uzalishaji wa malighafi tu
- Upungufu wa wataalamu na watu wenye ujuzi wa kisasa
- Utegemezi wa nje katika fedha na teknolojia
- Mabadiliko ya bei za bidhaa katika soko la kimataifa
- Ukosefu wa mtaji wa kutosha wa kuwekeza katika miradi ya maendeleo
Changamoto za Kijamii
- Mgawanyo wa kikabila na kireligio
- Ukosefu wa umoja baina ya watu wa Tanganyika na Zanzibar baada ya Muungano
- Ukosefu wa huduma za kijamii za kutosha vijijini
- Uhaba wa walimu na madaktari
- Ukosefu wa usawa wa kijinsia katika nafasi za uongozi
Changamoto za Kisiasa
- Uundwaji wa mfumo wa kisiasa uliojengwa kwenye misingi ya kidemokrasia
- Ushindani wa kisiasa baina ya makundi mbalimbali
- Uwezo mdogo wa serikali za mitaa
- Utekelezaji wa sera za kijamaa na kiuchumi
- Ushirikiano na ushirikishwaji wa wananchi wote katika mchakato wa maamuzi
Jinsi Tanzania Ilivyokabiliana na Changamoto Hizi
Serikali ya Tanzania ilichukua hatua mbalimbali kukabiliana na changamoto hizi:
- Kuweka misingi ya uchumi wa kujitegemea: Kupitia Azimio la Arusha na mikakati ya ujamaa
- Kukuza umoja wa kitaifa: Kupitia lugha ya Kiswahili, elimu ya siasa na michezo
- Kupanua elimu: Kupitia kampeni ya uelimishaji na uanzishwaji wa vyuo vya ufundi
- Kujenga uwezo wa kisiasa: Kupitia mfumo wa chama kimoja na uongozi wa Kiongozi Mkuu wa Nchi
- Kushirikiana kimataifa: Kupitia ushirikiano na nchi jirani na mashirika ya kimataifa
Zoezi la Marudio
- Fafanua maana ya "ujenzi wa taifa" na umuhimu wake kwa nchi iliyopata uhuru.
- Eleza mifumo minne mikuu iliyojengwa na Tanzania baada ya uhuru na mchango wake katika ujenzi wa taifa.
- Tofautisha kati ya mikakati ya ujenzi wa taifa na changamoto zilizokabili ujenzi huo.
- Fafanua jinsi Azimio la Arusha lilivyochangia katika ujenzi wa taifa la Tanzania.
- Eleza umuhimu wa elimu ya siasa katika ujenzi wa taifa baada ya uhuru.
- Chambua changamoto tano za kiuchumi zilizokabili Tanzania katika ujenzi wa taifa na jinsi zilivyokabilika nazo.
- Je, ni mafunzo gani Tanzania ya sasa inaweza kujifunza kutokana na uzoefu wa ujenzi wa taifa baada ya uhuru?
Kazi ya Kufanya 5.1
Fanya utafiti kuhusu mojawapo ya mikakati ya ujenzi wa taifa iliyotekelezwa na Tanzania baada ya uhuru (kwa mfano: Azimio la Arusha, uundwaji wa vijiji vya ujamaa, au kampeni ya uelimishaji). Andika ripoti fupi yenye kurasa 2-3 ukionyesha malengo, mafanikio na changamoto zilizokumbana na mkakati huo.
Kazi ya Kufanya 5.2
Kwa kutumia vyanzo mbalimbali vya habari (vitabu, makala za gazeti, au mtandao), andika insha yenye maneno 400-500 ukijadili juhudi za Tanzania katika kujenga taifa lenye maadili ya umoja, usawa na haki baada ya uhuru.
Sura ya Sita
Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
Utangulizi
Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya mwaka 1964 yalikuwa tukio muhimu la kihistoria ambalo liliathiri siasa, uchumi na jamii ya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla. Katika sura hii, utajifunza kuhusu dhana ya mapinduzi, chimbuko la Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, sababu za mapinduzi hayo na mchango wake katika maendeleo ya Zanzibar na Tanzania. Umahiri utakaoujenga utakuwezesha kuthamini na kuenzi juhudi za wapiganaji wa mapinduzi na kuchangia katika kudumisha maadili ya mapinduzi katika jamii.
Fikiri
Maana ya mapinduzi katika maendeleo ya jamii.
Dhana ya Mapinduzi
Mapinduzi ni mabadiliko makubwa na ya ghafla katika mfumo wa kisiasa, kiuchumi au kijamii wa nchi au jamii. Mapinduzi huchukua nafasi ya mfumo uliopo na mfumo mpya wenye maadili, kanuni na mifumo tofauti kabisa.
Mapinduzi yanaweza kuchukua njia mbalimbali:
- Mapinduzi ya kisiasa: Kubadilisha mfumo wa utawala na uongozi
- Mapinduzi ya kiuchumi: Kubadilisha mfumo wa uzalishaji na usambazaji wa mali
- Mapinduzi ya kijamii: Kubadilisha mfumo wa jamii na maadili yake
- Mapinduzi ya kiteknolojia: Kubadilisha mbinu za uzalishaji na mawasiliano
Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalikuwa mchanganyiko wa mapinduzi ya kisiasa, kiuchumi na kijamii yaliyolenga kubadilisha kabisa mfumo wa utawala na jamii ya Zanzibar.
Chimbuko la Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalitokea tarehe 12 Januari, 1964, chini ya uongozi wa John Okello, mwanamgambo aliyeongowa kundi la waasi wachache walioshambulia makambi mbalimbali ya kijeshi na kuwateka madaraka wakuu wa serikali ya Sultani.
Mkondo wa Matukio ya Mapinduzi
Zanzibar inapata uhuru kutoka kwa Waingereza chini ya Sultani Jamshid bin Abdullah
Wananchi wa Zanzibar wanaanza kuonyesha wasiwasi na serikali ya Sultani
Mapinduzi yaanza usiku kwa shambulio la kuvunja gereza na kuwafungulia wafungwa
Wapiganaji wa mapinduzi hushika kituo cha redio na kutangaza kushindwa kwa serikali ya Sultani
Sultani na wafuasi wake wakimbilia nje ya nchi
Baraza la Mapinduzi la Kisiwani Zanzibar lianzishwa chini ya Abeid Amani Karume
Mapinduzi haya yalikuwa na msukumo mkubwa kutoka kwa wananchi wa Kiafrika ambao walikuwa wameona uhuru wa Zanzibar mnamo Desemba 1963 kuwa haukuwaondolea ukandamizaji na ubaguzi ambao walikumbana nao chini ya utawala wa Waarabu.
Sababu za Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
Sababu za Kisiasa
Baada ya uhuru wa Zanzibar mnamo Desemba 1963, serikali ya Sultani ilikuwa imeundwa na vyama vya ZNP na ZPPP, ambavyo vilikuwa vinaongozwa na Waarabu. Hali hii ilisababisha:
- Uongozi uliobaki mkononi mwa Waarabu na wenyeji wa asili ya Kiajemi
- Kukosa uwakilishi wa kutosha kwa Waafrika katika serikali
- Kuendelea kwa mfumo wa kikoloni wa utawala
- Kutokuwa na usawa wa kisiasa kati ya makundi mbalimbali ya kijamii
Sababu za Kiuchumi
Uchumi wa Zanzibar ulikuwa umegawanyika kimatabaka, ambapo:
- Waarabu na Wahindi walikuwa na udhibiti wa biashara na sekta ya kilimo
- Waafrika walikuwa wakilima wadogo na wafanyikazi wa mashambani
- Kulikuwa na tofauti kubwa ya kimaisha kati ya makundi mbalimbali
- Ardh nzuri za kilimo zilikuwa mikononi mwa Waarabu na Wahindi
- Wafanyakazi Waafrika walilipwa ujira mdogo usioendana na kazi walizokuwa wakifanya
Sababu za Kijamii
Jamii ya Zanzibar ilikuwa imegawanyika kikabila na kidini:
- Waarabu na Wahindi walikuwa na hadhi ya juu katika jamii
- Waafrika walikuwa na hadhi ya chini na walibaguliwa
- Kulikuwa na ubaguzi katika upatikanaji wa huduma za kijamii kama elimu na afya
- Kulikuwa na mgawanyiko wa kijamii uliojengwa juu ya rangi na asili
Sheikh Abeid Amani Karume
Alikuwa kiongozi mkuu wa ASP na baadaye akawa Rais wa kwanza wa Zanzibar baada ya Mapinduzi. Alikuwa mwanasiasa mashuhuri na mwanaharakati aliyejitolea kwa maslahi ya Waafrika wa Zanzibar.
Kielelezo 6.1: Sheikh Abeid Amani Karume
Sheikh Abeid Amani Karume - Rais wa kwanza wa Zanzibar baada ya Mapinduzi
Wanaharakati na Viongozi wa Mapinduzi
Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yaliungwa mkono na kuongozwa na watu mbalimbali waliojitolea kwa ajili ya haki na usawa:
John Okello
Alikuwa kiongozi wa kijeshi wa mapinduzi na ndiye aliyeongoza shambulio la kwanza. Alikuwa mwanamgambo mwenye uzoefu wa kijeshi na aliwahi kuhudumu katika jeshi la Uganda.
Abdullah Kassim Hanga
Alikuwa mwanaharakati na mwanasiasa aliyejitolea kwa harakati za ukombozi. Alikuwa mwanachama muhimu wa ASP na alichukua nafasi muhimu katika mapinduzi.
Babu
Alikuwa kiongozi wa kisiasa na mwanaharakati aliyeongoza harakati za kisiasa za kupinga utawala wa Sultani. Alikuwa na uhusiano wa karibu na viongozi wengine wa mapinduzi.
Kielelezo 6.2: Baadhi ya viongozi walioshiriki Mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964
Baadhi ya viongozi walioshiriki Mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964
Mchango wa Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
Mabadiliko ya Kisiasa
Baada ya mapinduzi, mabadiliko makubwa yalifanyika katika mfumo wa kisiasa wa Zanzibar:
- Uanzishwaji wa Baraza la Mapinduzi la Kisiwani Zanzibar
- Kufutwa kwa utawala wa Sultani na kuanzishwa kwa jamhuri
- Kuundwa kwa serikali ya mapinduzi iliyolenga maslahi ya wananchi wengi
- Kuongezeka kwa ushiriki wa raia wa kawaida katika siasa
Kielelezo 6.3: Baraza la Kwanza la Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964
Baraza la Kwanza la Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964
Mabadiliko ya Kiuchumi
Mapinduzi yalileta mabadiliko makubwa katika uchumi wa Zanzibar:
- Mgawanyo wa ardhi kwa wakulima wadogo
- Uanzishwaji wa mashirika ya umma katika sekta mbalimbali
- Kuboreshwa kwa hali ya wafanyakazi na wakulima
- Kupunguzwa kwa tofauti ya kimaisha kati ya makundi mbalimbali
- Kuanzishwa kwa mfumo wa ushirika wa kiuchumi
Mabadiliko ya Kijamii
Mapinduzi yalichangia kubadilisha jamii ya Zanzibar:
- Kupunguzwa kwa ubaguzi wa kijamii na kikabila
- Kupanuliwa kwa haki za kijamii kwa wananchi wote
- Kuboreshwa kwa huduma za kijamii kama elimu na afya
- Kuongezeka kwa fursa za maendeleo kwa vijana na wanawake
- Kukuza utambulisho wa Kiafrika na kudumisha utamaduni wa asili
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalichangia kuharakisha muungano wa Tanganyika na Zanzibar:
- Mapinduzi yaliweka msingi wa kujenga uhusiano wa karibu na Tanganyika
- Viongozi wa Zanzibar na Tanganyika walianza majadiliano ya muungano mara tu baada ya mapinduzi
- Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulifanyika mnamo 26 Aprili, 1964 na kuunda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
- Muungano huu uliimarisha nchi katika kipindi kigumu cha ujenzi wa taifa baada ya ukoloni
Zoezi la Marudio
- Fafanua maana ya "mapinduzi" na tofautisha kati ya aina mbalimbali za mapinduzi.
- Eleza sababu za kisiasa, kiuchumi na kijamii zilizosababisha Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
- Fafanua jukumu la viongozi watatu waliochangia katika Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
- Taja na ueleze mabadiliko manne makuu yaliyotokana na Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
- Eleza jinsi Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalivyochangia katika kuunda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
- Chambua changamoto zilizokabili Zanzibar baada ya Mapinduzi na jinsi zilivyokabilika nazo.
- Je, ni mafunzo gani Tanzania ya sasa inaweza kujifunza kutokana na Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar?
Kazi ya Kufanya 6.1
Fanya utafiti kuhusu mojawapo ya viongozi wa Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar (kwa mfano: Sheikh Abeid Amani Karume, John Okello, au Abdullah Kassim Hanga). Andika wasifu wake ukiangazia maisha yake, mchango wake katika mapinduzi na athari ya uongozi wake kwa Zanzibar na Tanzania.
Kazi ya Kufanya 6.2
Andika insha yenye maneno 300-400 ukijadili jinsi Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalivyochangia katika kukuza maadili ya usawa, haki na umoja katika jamii ya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.

No comments
Post a Comment